Category: Maendeleo

DIRA YA TAIFA YA MAENDELEO 2050

Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050 (Dira 2050)

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania – Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050 (Dira 2050)

Read More
image

MUHADHARA WA WAZI WA KITAALUMA KUTOKA KWA WAKUFUNZI WA OFISI YA MWENDESHA MASHTAKA MKUU NCHINI URUSI

Faida ya muhadhara huu ni;

1. Kuongeza uelewa kwa umma

2.Kupambana na ufisadi na unyanyasaji wa mamlaka

3. Kongezwa kwa upana wa uelewa kwa vyombo vingine vya haki na sheria

Muhadhara huu kwa ujumla wake unaleta umuhimu katika kukuza uwajibikaji, uwazi na uelewa wa umma kuhusu masuala ya sheria na haki nchini Urusi na hata kwa mataifa mengine.

#SSH #CCM #KaziIendelee #Nchiyangukwanza #Sisinitanzania #Matokeochanya #MSLAC #SamiaSuluhuHassan #Katibanasheria

Read More

ZAIDI YA WATOTO 200 WAKUTWA WAKIPATIWA MAFUNZO YASIYO NA MAADILI,TAHADHALI WAZAZI WAONYWA

Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Halima Okash ameagiza kufungwa kwa Taasisi ya Mango Kinder iliyopo Kata ya Dunda Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani baada ya kituo hicho kukiuka utaratibu wa leseni yake ya kutoa haki kwa Watoto na badala yake kuwakusanya Watoto zaidi ya 200 na kuwapa elimu juu ya masuala mbalimbali ikiwemo yaliyo kinyume na maadili ya Mtanzania chini ya ufadhili wa Raia wa Ujerumani.

Kituo hicho huwakusanya Wanafunzi kuanzia saa nane mchana hadi saa 12 jioni na kuwapikia chakula kisha kuwafundisha masuala mbalimbali bila ya kibali ambapo DC Halima ameagiza pia kusitishwa kwa kibali cha Taasisi hiyo na leseni na ameitaka Kamati ya Usalama kuondoka na Mmiliki wa Taasisi hiyo Mtanzania Franky Silvester Neumann na Timu yake akiwemo Mke wa Franky ambaye ni Raia wa Ujerumani ili wakahojiwe zaidi.

Awali wakati wa mahojiani yake na DC, Franky amesema “Mimi nilikuwa Ujerumani nikawaambia Tanzania nina Watoto hali yao sio nzuri, wakanipa ufadhili Euro 1000 kila mwezi tuwe tunawapikia Watoto chakula, wakimaliza wanasoma msomo mbalimbali”

DC Halima amesema “Tumekuta zana mbalimbali ambazo inatupeleka kugundua Watoto hawafundishwi maadili mema na mengi ya mambo wanayofundishwa ni mambo ya kijinsia ambayo yanakiuka taratibu na mila na desturi zetu”.

“Nimeelekeza tutasitisha kibali na leseni ya Taasisi hii na wote wanaohusika na Taasisi tutaondoka nao kwa ajili ya mahojiano na uchunguzi zaidi lakini hili eneo halitotumika tena, hawa Watoto tangu November mwaka jana wanakuja hapa na Watu hawatoi taarifa kwa wakati, utamaduni wa kwetu wanaenda kuubadilisha”

Read More

KUTEULIWA NA RAIS HAKUTOWAFANYA WATEKELEZE MAJUKUMU YAO IPASAVYO.

Mkutano unahakikisha kuwa maoni ya vyama vyote vya siasa, na wananchi yanapewa uzito na kuzingatiwa katika kutengeneza sheria mpya. Ushirikiano wa wadau wote unaboresha uwazi na uwajibikaji, kuhakikisha kuwa mchakato wa kisheria unafanyika kwa njia inayowakilisha maslahi ya jamii

Read More

MATUMIZI YA MITANDAO KATIKA UCHAGUZI YAINGIE KATIKA SHERIA

MBUNGE wa Viti Maalumu, Neema Lugangira ameshauri Mswada wa Sheria ya Tume Huru ya Uchaguzi uwe na Ibara inayoongelea masuala ya Matumizi ya Mitandao katika Uchaguzi ikiwemo (Akili Mnemba – AI)

Read More

KATIKA HIZI 4R, TUANZE NA MARIDHIANO, NA YASIWE KATI YA CHAMA NA CHAMA BALI KATI YA WANANCHI.

“Kikombe tulichonyweshwa kuanzia mwaka 2015 hakuna Mtanzania ambaye atakisahau. Mimi ninavyoona hapa tuanze na maridhiano (reconciliation). Hizi R4 zifafanuliwe vizuri na Watanzania waelewe. Maridhiano yasiwe kati ya chama na chama, maridhiano yawe ni yawatanzania na siyo kati ya chama na chama. Naomba kuwe na semina maalum ya hizi R4 ili zieleweke” Bw. Joseph Thelasini.

Read More

HATUWEZI KUTENGENEZA NCHI CHINI YA MASHAKA

“Chochote kinaandikwa kwenye Sheria haipaswi kuwa na mashaka juu ya mamlaka ya Mhe. Rais. Hatuwezi kutengeneza nchi chini ya mashaka, ni vema kumuamini Rais chini ya vyombo vyake. Ni vema tuamini kuwa kuna Watumishi wa Umma ambao ni waaminifu maana wanapitia michakato. Tumesema kuwa Tume itakuwa huru, tumeshaandika kwenye sheria kuwa Tume itakuwa huru, hii inatosha hatuhitaji maneno mengine. Watumishi wasiwe waoga kwakuwa watu wengi wanasema kuhusu jambo Fulani (tunaondoa paradox), tutunze ustahimilivu (Resiliency)” Bw. Thabiti Mlangi;

Read More
JM

TATHIMINI YA KINA JUU YA MKUTANO MAALUM WA MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA NCHINI TANZANIA, UKIFAFANUA MJADALA MZIMA JINSI WADAU WALIVYOTOA NA KUCHANGIA MAWAZO YAO JUU YA MADA ILIYOWEKWA MEZANI 

(SIKU YA PILI)

UFUNGUZI 

 Mkutano ulianza na ufunguzi uliofanywa na Mhe. Othman M. Othman, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Kikao kilianza na salaam za utangulizi na viongozi mbalimbali, ikijumuisha Mhe. Jenista Mhagama, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu – Sera, Bunge na Uratibu.

 Mada kuu ya kikao ilikuwa mswada wa sheria za uchaguzi na vyama vya siasa, na matokeo ya kikao cha Baraza la Vyama vya Siasa kilichofanyika awali.

Maoni ya Wadau

Wadau mbalimbali walitoa maoni yao kuhusu mswada huo.

Bw. Majaliwa Kyala aliipongeza Serikali kwa kuondoa kifungu cha mgombea binafsi na kuelezea umuhimu wa kusimamia uchaguzi wa Serikali ya Mitaa.

Bi. Nuru Kimwaga aliipongeza Serikali kwa kuwaunganisha wanasiasa na kutoa wito wa kuhakikisha ushiriki wa wanawake katika Tume ya Uchaguzi.

Bw. Hassan Almasi alikumbusha historia ya miswada ya sheria na umuhimu wa kuzingatia maoni ya wadau.

Bi. Neema Lugangira alisisitiza umuhimu wa matumizi ya mitandao katika uchaguzi na kutoa wito wa kuimarisha usalama wa kadi za kupigia kura.

Prof. Ibrahimu Lipumba alitilia mkazo umuhimu wa kufanya marekebisho ili kutatua matatizo yaliyojitokeza katika uchaguzi wa mwaka 2020.

Mzee Cheyo alisisitiza umuhimu wa kuwa na Tume inayojali maoni ya wananchi na kutunza mila na desturi.

Bw. Abdul Nondo alitoa mapendekezo kadhaa kuhusu uteuzi wa wajumbe wa Tume ya Uchaguzi na jinsi ya kuboresha mswada.

Bw. Thabiti Mlangi alisisitiza umuhimu wa kumuamini Rais na kudumisha ustahimilivu wakati wa uchaguzi.

Majumuisho ya Maoni ya Washiriki

Dkt. ADA alitoa maoni kuhusu rushwa ya ngono na umuhimu wa kuwajengea uwezo wanawake.

Bw. Baruani Mshale kutoka TWAWEZA alipendekeza kuunganisha mswada na kufanya marekebisho kadhaa, ikiwa ni pamoja na kuhusu matumizi ya teknolojia.

Washiriki wengine walitoa mapendekezo kuhusu uteuzi wa wajumbe, sifa za wagombea, na mchakato wa kusikiliza kesi na rufaa.

Hitimisho

Kikao kilifungwa na Dkt. Doto M. Biteko, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati.

Mada zilizojadiliwa zilikuwa kuhusu sheria za uchaguzi na vyama vya siasa, na washiriki walitoa maoni yao kwa kina kuhusu mswada huo.

Mgeni rasmi alikuwa Bw. Othman Masoud Othman, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

HIVYO BASI 

Mjadala ulionyesha umuhimu wa kufanya marekebisho katika sheria za uchaguzi na vyama vya siasa ili kuboresha mchakato wa uchaguzi.
Kuna haja ya kuzingatia maoni ya wadau wote na kuhakikisha kwamba mabadiliko yanafanyika kwa njia inayosaidia demokrasia na usawa wa kijinsia.

Read More
MIKONO

TATHIMINI YA KINA JUU YA MKUTANO MAALUM WA MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA NCHINI TANZANIA, UKIFAFANUA MJADALA MZIMA JINSI WADAU WALIVYOTOA NA KUCHANGIA MAWAZO YAO JUU YA MADA ILIYOWEKWA MEZANI 

(SIKU YA KWANZA)

Mkutano ulilenga kuimarisha demokrasia na kuleta maridhiano kati ya vyama vya siasa. Kauli mbiu ya mkutano ilikuwa “Toa Maoni Yako Kuimarisha Demokrasia.” Baadhi ya mambo yaliyojadiliwa na wadau katika mkutano huo ni pamoja na dhana ya R4 (Reconciliation, Resiliency, Reforms, Rebuilding), misingi ya kutengeneza dira, na nafasi ya R4 katika kuleta utendaji mzuri wa hali ya kisiasa.

Watoa mada walisisitiza umuhimu wa maridhiano na uelewa wa pamoja kati ya vyama vya siasa, na kueleza kuwa tofauti za kiitikadi hazipaswi kuvunja umoja wa nchi. Pia, walijadili misingi ya kutengeneza dira, ikiwa ni pamoja na uhuru wa vyombo vya habari, uhuru wa kujieleza, kujenga upya, kuvumiliana, kusameheana, na maridhiano.

Watoa mada walisisitiza pia umuhimu wa kufanya marekebisho katika sheria za uchaguzi na sheria za vyama vya siasa. Waliongelea mabadiliko katika mifumo ya kisiasa, uchaguzi, na demokrasia, pamoja na kuanzisha mchakato wa kuandika katiba mpya. Waliomba pia uwiano wa jinsia na uwiano wa umri katika mchakato wa kisiasa.

Wakati wa majadiliano, wadau walitoa maoni yao kuhusu jinsi R4 zinavyoweza kuchangia katika maendeleo ya kitaifa, kufikia malengo ya Maendeleo Endelevu ya 2030 na Ajenda ya 2063. Walisisitiza umuhimu wa kuzingatia mabadiliko ya kiteknolojia na kufanya marekebisho katika mifumo ya elimu, siasa, na utamaduni ili iendane na uchumi wa nchi.

Mkutano pia ulijadili nafasi ya serikali, asasi za kiraia, na vyombo vya habari katika kusaidia utekelezaji wa R4. Baadhi ya washiriki walitoa maoni yao kuhusu jinsi wananchi wanavyoelewa R4 na umuhimu wa kuona matokeo ya sera na mikakati inayotekelezwa.

Katika mchana wa siku hiyo, washiriki walipata fursa ya kusikiliza mada kutoka kwa wataalamu na kutoa maoni yao kuhusu marekebisho ya sheria za vyama vya siasa na gharama za uchaguzi. Wadau walizungumzia changamoto zinazowakabili wanawake katika siasa, pamoja na kutoa mapendekezo ya kuboresha sheria na taratibu za uchaguzi.

Hitimisho la mkutano lilisisitiza umuhimu wa kulinda utulivu na kudumisha maridhiano, na washiriki walitoa ombi maalum kwa vyama vya siasa kuhusu marekebisho ya sheria na ushiriki wa wanawake katika siasa.

#IMARISHA DEMOKRASIA TUNZA AMANI

Read More
SAVE

NINI NAFASI YA SERIKALI, ASASI ZA KIRAI, NA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU HIZI R4 NA NINI KIFANYIKE?

Bw. Salim.

Niliposema ‘reform’ sikuwa na maana tuanze na reform. Hivyo ni lazima tuanze na maridhiano na kuvumiliana. Nakubaliana na wote wanaosema kuwa R4 ni falsafa sahihi sana. Hii mimi ninaamini kuwa hii itakuwa ni ‘legacy’ kwa mama Samia. Nini kifanyike, tuione Serikali ikifanya kwa vitendo, hili sio suala la kisiasa. Tunaona mabadiliko kwenye mabadiliko kwenye maeneo mbalimbali. Ingawa kwenye siasa kuna mkwamo kwenye Sheria za Uchaguzi na Katiba mpya. Asasi za kiraia ziwaeleze wananchi na kuwafundisha.

Bw. S.Wasira.

Vyombo vya Habari vifanye kazi yake ya kuelimisha umma kwakuwa vinasilikizwa na Wananchi. Nafasi ya Serikali ni haya yanayoendelea, Serikali iko kwenye usahihi. Tutazame ‘reforms’ kwenye maeneo yote kwa mfano elimu,  vyama vya siasa vina nafasi ipi.

Bw. Ado – ACT WAZALENDO.

Mchakato wa Katiba nchi siyo jambo la kusubiri, mchakato wa Katiba mpya na ukamilike mapema baada ya uchaguzi mkuu. Mhe. Rais hakuwa na shinikizo lolote baada ya kichapo cha mwaka 2020, kwa hiari yake akaamua kufanya mabadiliko. R4 itapimwa kwa vitendo, kila mmoja wetu ana wajibu. Ingawa yako mambo ambayo yameshajenga mambo ya kitaifa. Sisi kama ICT Wazalendo tumechambua mambo ambayo yameshatekelezwa. Mengi yapo kwenye ripoti ya kikosi kazi, hivyo yaendelea kutekelezwa.

Bi. Mongela.

S5 za Japani zimewezesha maendeleo ya Japani. Hivyo na hili la R4 tunapaswa kufanyia mkamkati, tunapaswa kuitengenezea dira ili iwe ya Taifa. Tumuombe Mhe. Rais tulitoe mkononi mwa Mhe. Rais kisha tukimbiee nalo. Mimi natoa mapendekezo hizi R4 ziwe za umma na ziweze kwenda hata kwenya familia. Naomba kuwe na muendelezo ya kufikisha kwa kila mtu yaani Methodolojia, tukumbatie vile ambavyo tumeshavifanyia kazi.

Bw. Doyo.

Naomba kuungana na Mhe. Lipumba, ni vema wenzetu wa Serikali wakalichukua hili.  Kuhusu ajenda 2063, Mhe. Rais ameruhusu mwanamke aongoze mwanamke mmojammoja kwenye baraza ili washiriki kisheria. Nawaomba tutumie R4 kwenye  mjadala huu.

Read More